Unafikiri vita ya Ukraine imechangia kuongeza gharama za maisha?,
huenda hufahamu kuhusu mwanamuziki
Beyounce, ambaye sasa analaumiwa kwa kuongeza gharama za maisha nchini Sweden.
Kuanza kwa (World Tours) ziara ya dunia ya mwanamuziki huyo Sweden
mwezi uliopita kumechangia ongezeko la wateja mahotelini na bei za vyakula hotelini,
takwimu za uchumi za nchi hiyo zimeonyesha.
Nchi ya Sweden imeshuhudia ongezeko la mfumuko wa bei uliofikia
asilimia 9.7 mwezi Mei, huku ongezeko la bei za hoteli kwa malazi na chakula
zikitajwa kuchangia kupanda kwa mfumuko huo wa bei.
Mchumi Michael Grahn wa Danske Bank, amesema kwamba anadhani
kwamba ziara ya muziki ya Beyounce imechangia kupanda kwa gharama za malazi na vyakula
kwenye hoteli nchini humo kutokana na ongezeko la wageni.
0 Maoni