Polisi waanza kufanyia kazi taarifa za Polepole kutekwa

 

Jeshi la Polisi Tanzania limesema limeanza kufanyia kazi taarifa za madai kuwa aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba Humphrey Polepole ametekwa ili kubaini ukweli wake.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Oktoba 6, 2025 na Jeshi la Polisi, imesema limeona taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kutoka kwa baadhi ya ndugu wa Polepole wakidai kuwa ametekwa.

Hata hivyo Jeshi la Polisi limesema linaendelea kumsubiri, Humphrey Polepole, kufika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ili kutoa maelezo kuhusu tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, Polepole alitumiwa barua ya wito kwa mujibu wa sheria, lakini hadi sasa hajajitokeza kama alivyotakiwa kufanya.



Chapisha Maoni

0 Maoni