CPA Kuji afungua Kikao Kazi cha Maafisa Rasilimali Watu na Utawala

 

CPA Musa Kuji, Kamishna wa Uhifadhi Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) leo Oktoba 1, 2025 amefungua rasmi kikao kazi cha maafisa rasilimali watu na utawala ndani ya taasisi mama ya uhifadhi.

 Kikao kazi hicho kilifanyika jijini Arusha kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi na kuandaa mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo ili Maafisa na Askari Uhifadhi wa TANAPA waweze kufanya kazi kwa ari na ufanisi ili Shirika liweze kufikia malengo yake.

Kikao hicho pia, kilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Shirika - Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Abdallah Kiwango, Mkuu wa Sehemu ya Utawala - Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Peter Butiku, pamoja na Mkuu wa Sehemu ya Utumishi na Rasilimali Watu - Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Cecilia Mtanga.

Ifahamike kuwa Idara ya Utumishi na Rasilimali Watu ni muhimu hasa katika kuhakikisha kuwa rasilimali ya adimu yenye vipawa na weledi tofauti (watumishi) wanakuwa na mazingira bora na wezeshi ya kutekeleza majukumu yao pasina mawaa.




Chapisha Maoni

0 Maoni