Rais Samia alipia tiketi 10000 mechi ya ufunguzi CHAN leo

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa tiketi 10000 zenye thamani ya Shilingi Milioni 20 kwa ajili ya mashabiki kuingia  Uwanja wa Benjamin Mkapa  kuishangilia timu ya Tanzania (Taifa Stars), itakayokabiliana na Burkina Faso katika mchezo wa kwanza wa Mashindano ya CHAN 2024  leo Agosti 02, 2025.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndg. Gerson Msigwa wakati akiwasilisha fedha hizo kwa kampuni ya N Card ambapo mashabiki watakaowahi watakabidhiwa.




Chapisha Maoni

0 Maoni