Muhimbili na Vodacom watoa huduma za matibabu bure kwa wakazi wa Tanga

 

Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na  Kampuni ya Vodacom imeanza kutoa huduma ya matibabu bila malipo kwa wakazi wa mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.

Huduma hizo zinatolewa katika viwanja vya  Chuo cha Ualimu Korogwe kuanzia Julai 21 hadi 23 2025 baada ya hapo timu hiyo itahamia mkoani Kilimanjaro.

Huduma zinazotolewa katika kambi hiyo ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya macho, afya ya kinywa na meno, magonjwa ya akina mama na afya ya uzazi, magonjwa ya ngozi, magonjwa ya afya ya akili, sukari na homoni, huduma za maabara, matumizi sahihi ya dawa pamoja na saratani ikiwemo tezi dume.

Chapisha Maoni

0 Maoni