Majaliwa ashiriki mbio za Great Ruaha Marathon

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ameongoza zoezi la kupasha misuli (warm up), baadaye kuzindua rasmi na kuongoza mbio za Great Ruaha Marathon leo Julai 05, 2025  Ibuguziwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Ruaha huku zikibeba Kauli Mbiu; “Tuko Tayari Kuvibe na Kutalii.”

Akizungumza katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa ameto wito kwa waratibu wa mbio hizo kuweka mikakati ya kuzifanya ziwe za kimataifa ili ziweze kukutanisha raia wa mataifa mbalimbali duniani.

Lengo la Mbio hizo ni kuhamasisha uhifadhi wa mazingira  wa Mto Ruaha Mkuu ambao ni uti wa mgongo wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na kuifanya jamii kuona umuhimu wa kulinda vyanzo vya maji na kuhimiza matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

Mbio hizo pia zimehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James viongozi waandamizi wa Mkoa na wilaya zake, Kamishna wa Uhifadhi TANAPA Musa Nassoro Kuji na viongozi waandamizi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.




Chapisha Maoni

0 Maoni