Miji na Majiji mbalimbali nchini Marekani imeshuhudia maandamano makubwa dhidi ya Rais Donald Trump, maandamano ambayo yameandaliwa na kikundi kijulikanacho kama "No Kings".
Waandamanaji hao
walijitokeza kwa wingi kupinga gwaride la kijeshi lililoandaliwa jijini
Washington DC, tukio ambalo ni nadra kufanyika, na lilifanyika sambamba na siku
ya kuzaliwa kwa Trump.
Gwaride hilo pia
lililenga kuadhimisha miaka 250 tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Marekani.
Maandamano hayo
yamekuja baada ya wiki ya maandamano makubwa yaliyofanyika Los Angeles na
maeneo mengine, watu wakilalamikia sera kali za uhamiaji za utawala wa Rais Trump.
Katika majiji kama
New York, Philadelphia na Houston, wabunge, viongozi wa vyama vya wafanyakazi
na wanaharakati mbalimbali walihutubia umma uliojumuika kwa maelfu huku
wakipeperusha bendera za Marekani na mabango yenye ujumbe mkali wa kumpinga
Trump.
Katika onyo kali
kabla ya gwaride hilo lililofanyika Jumamosi jioni, Rais Trump alitahadharisha
kuwa maandamano yoyote yangekabiliwa na "nguvu kubwa".
0 Maoni