Raba ya Kimono inayouzwa kiasi cha shilingi 870,000


Kampuni ya viatu ya Japan ya Potato Limited imeuteka ulimwengu viatu kwa ubunifu wa raba yake inayojulikana sokoni kwa chapa ya Tokyo Kimono Shoes inayouzwa dola za Marekani 325. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Shotaro Kawamura anatengeneza raba hizo kwa kutumia kitambaa cha vazi la utambulisho wa kitamaduni Japan la kimono, ambalo huvaliwa mara chache siku hizi. 

Kwa kawaida vazi hilo hutumika tu katika hafla rasmi, na mara nyingi huhifadhiwa kwa vizazi, na wachambuzi wanadhani kuwa kuna mabilioni ya dola ya thamani ya mavazi ya kimono yaliyohifadhiwa na yasiyotumika katika makabati ya Wajapani. 

“Kwa kubadilisha muundo ili tuweze kutumia vitambaa vya kimono katika maisha ya kila siku, tunaweza kuhifadhi utamaduni kwa njia tofauti,” alisema Kawamura.

 Kwa mujibu wa Kawamura, kimono moja inaweza kutumika kutengeneza jozi 20 za viatu, ambavyo huuzwa kwa wateja duniani kote, kwa bei ya takriban dola za Marekani 325 kwa  jozi. 

Je, umeshawahi kufikiria kuwa unaweza kununua jozi moja ya raba kwa dola 325 ambayo ni sawa na karibu shilingi 870,000 za Tanzania.




Chapisha Maoni

0 Maoni