Katika kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya
Sita za kuboresha huduma za afya nchini Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila
imenza kambi maalum ya upasuaji wa upandikizaji wa meno bandia kwa njia ya
kisasa kwa wagonjwa ambao wamepoteza meno yao kutokana na sababu mbalimbali.
Akizungumza wakati wa kambi hiyo Daktari Bingwa wa Afya ya
Kinywa na Meno MNH. Mloganzila Dkt. Peter Shempemba amesema wagonjwa watakao
hudumiwa katikakambi hiyo ni pamoja na wale ambao walifanyiwa upasuaji mwishoni
mwa mwaka jana na wale ambao wanakuja kwa mara ya kwanza.
Ameongeza kuwa kundi la kwanza ni wale ambao
walishawapandikiza mizizi ya meno katika awamu ya kwanza na kipindi hiki
watapandikizwa meno na kundi lingine ni wale ambao wanapandikizwa mizizi kwa
mara ya kwanza.
“Upandikizaji huu ni wa ubora wa hali ya juu, meno tunayoyapandikiza
hayana tofauti na meno ya asili kwakuwa yanapandikizwa moja kwa moja kwenye
mfupa wa taya na yanadumu kwa muda
mrefu, hayawezi kutoka kirahisi, mtu ataweza kutafuna vizuri kama kawaida ”
amesema Dkt. Shempemba.
Kambi hiyo inafanyika kwa kushirikiana wataalam wa ndani na
Daktari Bingwa aliyebobea katika Upasuaji wa Taya kutoka Hospitali za Wochhardt
Dkt. Chirag Desai ambapo itafanyika kwa kipindiki hiki cha siku saba kuanzia
tarehe 20 hadi 26 Februari, 2025 ambapo takribani wagonjwa 45 watafanyiwa
upandikizaji.

0 Maoni