Rais Samia afanya uteuzi wa viongozi mbalimbali

 

Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali ambapo amemteua Prof. Mpoki Ulisubisya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI).

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, imesema Rais Samia pia amemteua Bi. Joyce Gideon Mapunjo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).



Chapisha Maoni

0 Maoni