Rais Samia afanya uteuzi wa mawaziri na viongozi wengine

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameirejesha Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kumteua Prof. Palamagamba Kabudi kuwa waziri wa wizara hiyo.

Taarifa ya Ikulu aliyoitolewa leo na Katibu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka kufuatia uteuzi wa viongozi mbalimali, Rais Samia amemteua, Gerson Msigwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Msigwa licha ya kuwa Katibu Mkuu ameongezewa jukumu la Usemaji Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Thobias Makoba aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ameteuliwa kuwa Balozi na atapangiwa kituo cha kazi.

Rais Samia pia, amemteua Mhe. Jerry Silaa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Damas Ndumbaro ameteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria huku Mhe. Hamad Masauni akiteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Uteuzi wa viongozi wote upo kwenye taarifa ya Ikulu hapo chini:-





Chapisha Maoni

0 Maoni