Rais Mwinyi atunukiwa Shahada ya Heshima Zanzibar

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Hussein Ali Mwinyi ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Zanzibar.

Chuo Kikuu cha Zanzibar kimemtunuku  Shahada hiyo ikiwa ni kutambua   na kuthamini Mchango  wa Uongozi wake  Unaoacha Alama  na historia itakayokumbukwa  wakati wote.

Hafla ya kutunukiwa Shahada hiyo imefanyika jana tarehe 5 Desemba 2024 katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu wakati wa Mahafali ya 22 ya Wahitimu wa mwaka 2024.

Shahada hiyo ya Heshima ya Uchumi  ametunukiwa kuthamini Mchango wake na Mafanikio makubwa yaliofikiwa Zanzibar hususan  Ukuaji wa Uchumi na Maendeleo yaliopatikana Kipindi kifupi cha Uongozi wake wa miaka minne  akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Rais Dk Mwinyi amekishukuru Chuo hicho kwa kuthamini juhudi na kazi anazofanya kwa ajili ya Maendeleo ya nchi.

Aidha Rais Dk.Mwinyi amebainisha kuwa Shahada hiyo aliotukuwa inaakisi kazi nzuri inayoifanya na Serikali anayoiongoza na itamuongezea hamasa ya Maendeleo zaidi.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi ameahidi kuienzi heshima hiyo na kuwahakikishia wananchi kuendelea kuwatumikia kwa uwezo wake wote na sio mwisho wa safari bali mwanzo wa hatua kubwa ya maendeleo yajayo.



Chapisha Maoni

0 Maoni