Taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma TANROADS
Tunapenda kufafanua taharuki iliyozuka kwenye mitandao
ya kijamii kuhusu Askari Monument ya Dar es Salaam.
Ni kwamba ujenzi unaoendelea katika Mradi BRT Awamu ya Tatu
hautaondoa wala kugusa SANAMU YA ASKARI iliyopo makutano ya Mtaa wa Azikiwe na
Samora.
Hata hivyo, kutokana na ufinyu wa eneo la barabara katika
makutano hayo, duara la bustani litapunguzwa bila kuathiri hadhi ya sanamu hiyo
na usalama wa matumizi ya barabara.
0 Maoni