Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan ameongeza bajeti kwa ajili ya ujenzi wa barabara za ndani katika wilaya
ya Ruangwa kutoka shilingi Bilioni 1 hadi shilingi bilioni 4.8
“Niwape Siri, Rais Dkt. Samia ametuunganisha Masasi na Ruangwa kupitia ujenzi wa barabara
ya Nanganga-Ruangwa na Km 38 zimejengwa pia ametupa fedha kwa ajili ya
kuunganishwa Ruangwa na Nachingwea kwa kiwango cha lami,” alisema Mhe.
Majaliwa.
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa amesema hayo leo Desemba 29,2023 wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Litama, Ruangwa mkoani Lindi.
0 Maoni