Kombora la roketi la Urusi limepiga jengo la makazi magharibi
mwa mji wa Ukraine, Lviv, na kuua watu wapatao wanne, Waziri wa Mambo ya Ndani
wa Ukraine amesema.
Waziri huyo Ihor Klymenko, ameongeza kuwa watu wengine 32,
wamejeruhiwa katika kile Meya wa Lviv alichokiita moja ya mashambulizi makubwa
yaliyowalenga raia katika makazi yao.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameapa kulipiza kisasi kwa
shambulizi hilo la usiku lililofanywa na “magaidi wa Urusi”.
0 Maoni