MISIME: Hatujawahi kupuuza ripoti za utekeji, tunapeleleza zingine zipo mahakamani

 

Jeshi la Polisi nchini limetangaza mafanikio makubwa katika kushughulikia matukio ya kihalifu nchini, likisisitiza kuwa kwa sasa lina uwezo zaidi na linafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu kutokana na kuwezeshwa na Serikali.

Akizungumza chombo kimoja cha habari hapa nchini, kuhusu kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime alifafanua kuwa ripoti za upotevu na utekaji hazipuuzwi na kwamba juhudi kubwa zimekuwa zikifanya kufichua uhalifu huo na kuwatia mbaroni wahusika.

 "Si kweli kwamba tukipatiwa ripoti hatuzifanyii kazi. Tunazifanyia kazi. Kiutekelezaji ni suala la muda tu; halafu mtuhumiwa atakamatwa," alisema.

Msemaji huyo alibainisha kuwa kuna matukio zaidi ya 86 yaliyokuwa na maelezo ya kupotea na kutekwa ambayo yameshughulikiwa. Katika matukio hayo, watu kadhaa wamekamatwa na kufikishwa mahakamani, huku wengine wakiwa tayari wamepewa hukumu.

Alisema vyombo vya habari vinapaswa kuwa na kumbukumbu katika matukio hayo na kazi iliyofanywa na jeshi la polisi kwa kuwa ndio wanaopelekewa taarifa kwa ajili ya kuzifikisha kwa umma kuonesha maendelea ya mashauri mbalimbali yaliyokuwa yanatafutiwa ufumbuzi na jeshi hilo.

Katika mazungumzo yake aliyataja baadhi ya  mashauri ambayo yalikuwa na dhana ya kupotea au kutekwa na polisi baada ya upelelezi ikabaini kwamba kulikuwa na uhalifu kutokana na imani za kishirikina, wivu wa mapenzi na mauaji yanayohusiana na mirathi au biashara.

Misime aliyataka mauji ya watu 11 Singida, mauaji ya mfanyabiashara Njombe na mauaji ya mke yaliyofanywa na mume huko Kigamboni.

Chapisha Maoni

0 Maoni