Benki ya CRDB imetangaza kuwa itafunga huduma zake zote kwa muda wa siku tatu mfululizo, kuanzia Ijumaa ya Septemba 5 hadi Jumapili ya Septemba 7, 2025, ili kutoa nafasi kwa maboresho ya mifumo ya kiteknolojia.
Taarifa
rasmi iliyotolewa leo kwenye akuanti ya CRDB na uongozi wa benki hiyo, imeeleza
kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wateja
kupitia maboresho yatakayofanywa na wataalamu wa ndani na nje ya nchi.
"Tunafahamu
kuwa hatua hii inaweza kuleta usumbufu kwa wateja wetu, lakini ni muhimu kwa
ajili ya kuboresha huduma na kuhakikisha usalama wa miamala," imeeleza
sehemu ya taarifa hiyo.
Katika
kipindi hicho cha siku tatu, huduma zote za benki hazitapatikana kwa namna
yoyote ile. Hii inajumuisha huduma katika matawi yote ya CRDB, mawakala wa
benki (CRDB Wakala), mashine za kutolea pesa (ATM), pamoja na huduma za
kidijitali kama SimBanking, Internet Banking, na miamala ya benki kupitia
mitandao ya simu.
Aidha, benki
hiyo imefafanua kuwa huduma zitaanza kuzimwa rasmi kuanzia saa sita usiku wa
kuamkia Septemba 5, ambapo kutakuwa na kukatika kwa huduma kwa muda wa saa
mbili, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maboresho hayo.
CRDB imetoa
wito kwa wateja wake kupanga shughuli zao mapema kabla ya tarehe hizo ili
kuepuka usumbufu. Aidha, imesisitiza kuwa huduma zitarudi kama kawaida kuanzia
Jumatatu, Septemba 8, mara baada ya maboresho kukamilika.
0 Maoni