TARURA yawajengea uwezo watumishi wapya wa kada mbalimbali

 

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imetoa mafunzo  elekezi ya kuwajengea uwezo watumishi wapya 98 wa kada  ya Uhandisi, Fundi Sanifu, Maofisa Hesabu, Wachumi pamoja na Ununuzi na Ugavi.

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Jiji-Mtumba katika Mji wa Serikali  jijini Dodoma.

Mafunzo hayo yaliongozwa na Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Bi. Azimina Mbilinyi akishirikiana na Idara nyingine TARURA Makao Makuu.

Pamoja na hayo watumishi hao wapya walitakiwa kufanya kazi kwa weledi na ufanisi na kufuata maadili ya utumishi wa umma wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.

Katika mafunzo hayo  watumishi hao walipatiwa mada nyingine kuhusiana na  sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma pia walikula viapo vya uadilifu wa utumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.




Chapisha Maoni

0 Maoni