Coca-cola ya Marekani kuanza kutumia sukari halisi ya miwa

 

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa kampuni ya Coca-Cola imekubali kutumia sukari halisi ya miwa katika vinywaji vyake vinavyouzwa Marekani.

Kwa sasa, Coca-Cola hutumia shira ya mahindi katika bidhaa zake za Marekani, lakini Waziri wa Afya, Robert F. Kennedy Jr., ameeleza wasiwasi wake kuhusu athari za kiafya za kiambato hicho.

"Nimekuwa nikizungumza na Coca-Cola kuhusu kutumia sukari halisi ya miwa katika Coke inayouzwa Marekani, na wamekubali kufanya hivyo," Trump ameandika kwenye mitandao ya kijamii. "Ningependa kuwashukuru wote walioko madarakani ndani ya Coca-Cola."

Ingawa Coca-Cola haikuthibitisha wazi mabadiliko hayo ya mapishi, Msemaji wa Kampuni hiyo alisema wanathamini "hamu na shauku ya Rais Trump" na kuongeza kuwa "maelezo zaidi kuhusu bidhaa mpya na bunifu katika safu yetu ya Coca-Cola yatatangazwa hivi karibuni."

Katika chapisho lake la Jumatano kwenye Truth Social, Trump alisema: "Hii itakuwa hatua nzuri sana kwao , utaona. Ni bora zaidi tu!"

Wakati Coke inayouzwa Marekani huwa inatumia utamu wa shira ya mahindi, Coke kutoka nchi nyingine kama vile Mexico, Uingereza na Australia mara nyingi hutumia sukari ya miwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni