CHADEMA hakijasaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi 2025

 

Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhani Kailima amesema vyama vya siasa 18 vya vimeridhia kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani kwa mwaka 2025 na hivyo kupata sifa ya kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba mwaka huu sambamba na chaguzi nyingine zote ndogo zitakazofanyika ndani ya miaka mitano ijayo.

Akizungumza katika hafla ya kusaini kanuni za maadili, Kailima ameeleza  wajibu wa kusaini kanuni za maadili ya uchaguzi kwa mujibu wa kifungu namba 162(2) cha sheria hiyo pamoja na aya ya 1.2 ya kanuni za maadii ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za mwaka 2025, kanuni  zinapaswa kusainiwa na wahusika kwa kila chama cha siasa, serikali na Tume.

Kailima amevitaja vyama hivyo vilivyotia saini Kanuni za Maadili ya Uchanguzi Mkuu 2025 kuwa ni chama cha AAFP, ACT WAZALENDO, ADA-TADEA, ADC, CCK, CCM, CHAUMA, CUF, MAKINI, DP, NCCR-Mageuzi, NLD, NRA, SAU, TLP, UDP, UMD na UPDP.

Ameeleza kwamba chama kimoja tu cha siasa ambacho hakijatia saini Kanuni za Maadili ya Uchanguzi Mkuu 2025 ambacho amekitaja kuwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kati ya vyama 19 vilivyosajiliwa.

Kailima amesema chama ambacho hakijasaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi leo hakitaruhisiwa kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu na chaguzi zote zitakazitokea katika kipindi cha miaka mitano ikiwemo uchaguzi mdogo.


Chapisha Maoni

0 Maoni