Siogopi mashujaa wa mitandaoni- Lissu

 

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Tundu Lissu, amesema maneno ya baadhi ya watu wanaomshambulia mitandaoni hayamuogopeshi asiendele na majukumu yake ya kisiasa.

“Maneno yao hayaniogopeshi, mimi natembea na risasi mgongoni hivyo siwezi kutishwa na maneno ya mashujaa wa mitandaoni,” alisema Lissu.

Lissu alikuwa akijibu maswali aliyoulizwa na waandishi wa habari leo Desemba 10, 2024, Jijini Dare s Salaam kuhusiana na mashambulizi ya maneno mitandaoni yanayofanywa dhidi yake.

 “Mimi natembea na risasi mgongoni, nitaogopa mawe ya mitandaoni ?, natembea na risasi ipo hapa mgongoni nitaogopa nanii?, Niliitwa mhaini na wakatumwa watu mnafahamu yaliyoendelea, sasa nitaogopa hawa mashujaa wa mitandaoni,” alihoji Lissu.

Chapisha Maoni

0 Maoni