Jitihada za kurejesha miundombinu iliyoathiriwa mvua zinaendelea katika Daraja la Kizangaze lililopo Wilayani Same ambapo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu pamoja na Kamati ya Usalama ya Mkoa na wataalam tayari amekwisha wasili kuhakikisha zoezi hili linakamilika kwa wakati.
Daraja hili linaunganisha kata ya Maore na Ndungu
zilizopo Wilayani Same ambapo mawasiliano yamekatika kwa muda kati ya kata hizo
mbili kutokana athari ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Wilayani humo.



0 Maoni