Ahadi ni deni, Mhe. Mathayo atimiza ahadi zake Same

 

Mbunge wa Same Magharibi, Mhe. David Mathayo, amerejea kwa wananchi wake kutekeleza ahadi kwa kutoa mifuko 100 ya saruji ya kujenga nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi Nasuru, shilingi 1,760,000 kwa ajili ya madirisha ya nyumba ya mwalimu pamoja na mabati hamsini ya nyumba hiyo.

Pia, Mhe. Mathayo amekabidhi shilingi 2,000,000 kwa ajili ya milango ya nyumba hiyo ya mwalimu, shilingi 350,000 kwa ajili ya kununua kipimo cha Zahanati, shilingi 400,000 kwa ajili ya pumpu ya kumwagilia bustani ya mbogamboga ya kikundi cha vijana.

Kama hiyo haitoshi, Mhe. Mathayo ameahidi kuwasomesha vijana wanaotaka kusomea cheti cha udereva wa malori ili waweze kupatiwa leseni ya udereva wa malori, na kuwaahidi kwamba watakapo faulu na kupata leseni atawaajiri kwenye kampuni yake.

“Kesho asubuhi mmoja wenu au kiongozi wenu mtakayemchagua aje mimi nitawapatia shilingi laki nne kila mmoja ili mkasomee mje niwajiri kwenye kampuni yangu, kwa sababu mimi nataka vijana waaminifu, nawapo niliowachukua kutoka hapa Nabangalala wako huko nafanyanao kazi,” alisema Mhe. Mathayo.

Kwa upande wao vijana hao wamemshukuru mbunge wao huyo kwa kuwawezesha kwenda kupata elimu itakayowasaidia kuweza kupata leseni ya kundesha malori kwa kuwa kilichokuwa kinawakwamisha ni fedha za kusomea cheti licha yao wao kujua kuendesha malori.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria kikao cha mbunge huyo wamempongeza kwa kutimiza ahadi mbalimbali anazotoa na kusaidia kuboresha shughuli za maendeleo na kiuchumi za wapiga kura wake wa jimbo la Same Magharibi.




Chapisha Maoni

0 Maoni