Wanakijiji wa Nyasaunga kutumia Zahanati yao ifikapo Desemba

 

Wanakijiji wa Kijiji cha Nyasaungu wameanza kuwa na matumaini ya kupata huduma ya matibabu katika Zahanati yao ifikapo Desemba mwaka huu, baada ya ujenzi wake kukamilika.

Taarifa iliyotolewa na Mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo imesema kijiji hicho chenye vitongoji vitano kwa sasa kinakamilisha ujenzi wa Zahanati yake.

Kijiji hiki ni moja ya vijiji vitatu vya Kata ya Ifulifu, vijiji vingine ni Kabegi na Kiemba ambavyo kila kimoja kina zahanati yake, imeeleza taarifa hiyo.

“Kwa hiyo, ifikapo Desemba 2024, kila kijiji ndani ya Kata ya Ifulifu kitakuwa na zahanati yake, hatua kubwa sana ya maendeleo kwenye Kata hii,” Imesema taarifa ya Prof. Muhongo.

Taarifa hiyo imeeleza vyazo vya fedha vya Zahanati ya Nyasaungu kuwa ni michango ya wanakijini na mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo.

Katika kufanikisha upatikanaji wa fedha hizo Prof. Muhongo alipiga Harambee mbili za kupata fedha za kuanza ujenzi wa zahanati hiyo. Wanakijiji wanachangia nguvukazi.

Pamoja na vyanzo hivyo, pia Serikali Kuu imechangia jumla ya shilingi milioni 100.

Chapisha Maoni

0 Maoni