Mkuu wa Mkoa
wa Simiyu, Kenani Kihongosi, ameongoza vyama vya siasa vya upinzani 19 mkoani
Simiyu kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali mkoani humo, pamoja na kupata
nao chakula cha pamoja.
Katika ziara
hiyo RC Kihongosi amewasisitiza viongozi wa vyama vya siasa Simiyu kudumisha
umoja, upendo na mshiakamno katika mkoa huo kwa kuzingatia kuziishi 4R za Mhe.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
RC Kihongosi
ametumia fursa hiyo kuwaeleza viongozi wa vyama vya siasa mkoani Simiyu kuwa
yeye na viongozi wenzake wameteuliwa na Rais Dkt. Samia kuwatumikia wananchi na
miradi yote wanayotekeleza ni yakwao na kwa kuwa ni yakwao ni lazima waijue.
“Lazima
viongozi wa siasa mjue miradi imegharimu shilingi ngapi, lakini pia mjue kuwa
miradi hii inakwenda kutatua shida za wananchi wenu mnaowaongoza katika jamii,
kwahiyo nyinyi mtusaidie kwenda kuwatuliza wananchi mkahubiri amani,” amesema
Kihongosi
0 Maoni