Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.
Jakaya M. Kikwete amesema Rais Samia Suluhu Hassa anapaswa kupongezwa kwa
kubeba mzigo mzito katika kukamilisha mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar
es Salaam hadi Dodoma, huku vipande vingine vikiwa katika hatua mbalimbali za
utekelezaji.
Akijibu swali la Idriss Sultan katika Podcast maalumu
iliyofanyika nyumbani kwake, Rais huyo wa awamu ya nne wa Tanzania, amesema
kuwa wazo la SGR lilianza baada ya Mkapa kufanya mazungumzo na Rais Kagame wa
Rwanda juu ya kujenga reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Kigali.
Hata hivyo Kikwete amesema tumpongeze Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kubeba mzigo mzito katika kukamilisha mradi huo utakaogharimu takriban Dola bilioni 7 za kimarekani.
0 Maoni